JUMUIYA
ya wanafunzi wa Elimu ya Juu Wanachadema Mkoa wa Iringa (CHASO)
wamelaani vikali mwenendo mbovu wa Bunge Maalum la Katiba katika
kuendesha na kujadili rasimu ya katiba tangu lilipoanza kwa kuendesha
malumbano kila kwenye kikao na wakati mwingine wajumbe kuzomeana na
kuacha kujadili mambo ya msingi yanayowagharimu Watanzania mamilioni ya
Fedha.
Wakitoa
msimamo mbele ya waandishi wa habari katika ofisi za Chaso zilizoko
Tumaini katika kata ya Kihesa jana, Katibu Mwenezi wa Chaso Iringa,
Michael Noel alisema bunge la katiba limepoteza imani kwa wananchi na
wamekuwa wakilipwa posho kwa kodi zetu, wanataka watupatie katiba ya
msimamo wa chama cha mapinduzi.
Alisema
kuwa chaso haiko tayari kuona mawazo ya wananchi katika rasimu ya
katiba yanapotoshwa kwa misingi ya faida ya chama kimoja hivyo wako
tayari kuandamana nchini nzima endapo ccm watapitisha katiba yenye
msingi ya maslahi ya chama chao.
MJUMBE Sr
Post a Comment