Bingwa wa
zamani wa mbio za magari ya langalanga ya F1, Michael Schumacher
ameanza kuonyesha hali ya kupata fahamu baada ya miezi kadha ya kuwa
katika hali ya kutojitambua.
Wakala
wake Sabine Kehm amesema katika taarifa yake kwa vyombo vya habari
amesema Schumacher "anaendelea vizuri", akisema kwamba wana "uhakika"wa
kupona kwake.
Madaktari nchini Ufaransa wanafanya jitihada za kumwondoa katika hali ya kutojitambua, bingwa huyo mara saba wa F1.
MJUMBE Sr
Post a Comment