Viongozi
wakijadiliana wakati wa zoezi la kuweka Alama muhimu za barabarani
Katikati ya Jiji tayari kwa mabadikiko ya mielekeo ya barabara za Samora
na Sokoine unaoanza Jumatatu 28/04/2014.
Vijana wakiweka kibao cha alama barabarani.
Jana
Aprili 26, 2014 zoezi la kuweka Alama muhimu Katikati ya Jiji la Dar es
Salaam limekamilika tayari kwa mabadikiko ya mielekeo ya barabara za
Samora na Sokoine unaoanza Jumatatu 28/04/2014. Kwa daladala itakuwa
kama ifuatavyo:
Habari na Picha na Deo Mutta, DART
1.
Daladala Zote zinazotokea Barabara ya Ally Hassan Mwinyi zitaingia
mjini kupitia Bibi Titi na kukata kushoto kuingia barabara ya Makataba
na kuishia Posta Mpya na kutoka kwa kuzunguuka Mnara wa Askari na
kushuka na Maktaba na Kupinda kulia kuingia Bibi Titi na baadaye All
Hassan Mwinyi.
2.
Daladala Zote zinazotokea Barabara ya Morogoro zitapinda kushoto
kuingia Bibi Titi na Kupinda kulia kuingia Maktaba hadi Posta Mpya.
Zitatoka kwa kuzunguuka Mnara wa Askari na kuingia Samora hadi Clock
Tower na kuingia Uhuru na Kupinda kulia kuingia Bibi Titi na Kupinda
kushoto kuingia Morogoro.
3.
Daladala zinazotokea Barabara ya Uhuru zitakwenda moja kwa moja hadi
Clock Tower na kuingia Barabara ya Railway na Kupinda kushoto kuingia
Sokoine na kuishia Stesheni. Zitatoka kwa kupitia Samora kutokea station
na kuingia Uhuru kupitia mnazi mmoja.
4.
Daladala zinazotokea Barabara ya Nyerere zitapita bibi Titi na kukunja
kulia kuingia Uhuru hadi Clock Tower na kuingia Railway na kukunja
kushoto kuingia Sokoine na kuishia Stesheni. Zitatoka kupitia Samora
hadi Clock Tower na kuingia Nkurumah na kuingia Nyerere eneo la Cocabs.
5.
Daladala zinazotokea barabara ya Kilwa Zitapitia Sokoine na kuishia
Stesheni na kutoka kupitia Railway na kuingia Sokoine kuelekea Water
Front.
Ufafanuzi Zaidi!
MABADILIKO
YA UELEKEO WA BARABARA KATIKATI YA JIJI LA DAR ES SALAAM KUANZIA SIKU YA
TAREHE 28/04/2014. TRAFFIC CIRCULATION AT CBD
1. Kipande
cha Mtaa wa Samora kuanzia Mnara wa Askari (Askari Monument) hadi Clock
Tower Magari kutakuwa na mabadiliko ambayo magari yatakuwa yanaelekea
Clock Tower badala ya Askari Monument.
2. Barabara
ya Sokoine kuanzia Station hadi Makutano ya Mtaa wa Maktaba Posta Ya
Zamani Magari yatakuwa yanaelekea Uelekeo mmoja wa Station Posta ya
Zamani tofauti na ilivyo sasa Posta ya Zamani kwenda Station.
3. Barabara ya Kivukoni Kuanzia Posta ya Zamani hadi Ferry itakuwa barabara ya mielekeo miwili (Two Ways).
4. Barabara ya Samora kuanzia Mnara wa Askari hadi Ocean Road Hospitali itakuwa ni barabara ya mielekeo miwili.
5. Daladala
Zote zitakazotokea barabara za Makataba zitakunja kulia pembeni ya Jengo
la NBC na hadi Makutano ya Mkwepu na kukunja kushito kuingia Sokoine
pale Posta ya Zamani na baadaye kukunja kushoto kuingia Makataba na
kurudi Posta Mpya .
Key:
1. RANGI YA NJANO - Njia ya Uelekeo Mmoja {One Way}.
2. RANGI YA BLUE MPAUKO - Njia ya Mielekeo Miwili {Two Way}
3. RANGI YA KIJANI - Mitaa ya Kutembea kwa Miguu Magari marufuku {Walking Streets}
4. RANGI NYEKUNDU - Barabara za kupita Daladala
5. RANGI YA BLUU ILIYOIVA - Barabara za DART
6. DUARA ZA NJANO - Mzunguuko {Roundabout}
7. MSALABA WA KIJANI - Makutano yenye Taa za kuongozea Magari {Singnalized Intersection}
Kwa Maelezo zaidi Wasiliana na Ofisi za DART
UBUNGO PLAZA GHOROFA YA KWANZA.
AU.
OFISI YA MHANDISI WA MANISPAA YA ILALA
MJUMBE Sr
Post a Comment