Unknown Unknown Author
Title: CHATU ATIKISA JIJI LA MBEYA;WAGANGA WA KIENYEJI WAHUSISHWA!
Author: Unknown
Rating 5 of 5 Des:
5 SIKU chache baada ya uongozi wa jiji la Mbeya kutoa tahadhari juu ya uwepo wa nyoka mkubwa aina ya chatu katika eneo...
SIKU chache baada ya uongozi wa jiji la Mbeya kutoa tahadhari juu ya uwepo wa nyoka mkubwa aina ya chatu katika eneo la Rift Valley lililopo pembezoni mwa mto Meta jijini humo chatu mtoto amekamatwa na kuzidisha tishio la nyoka huyo FikraPevu imefahamishwa.
Kumbukumbu zinaonyesha kuwa tahadhari ilitolewa na Mkurugenzi wa Halmashauri ya jiji la Mbeya, Mei 14, 2014 kuwatahadharisha wananchi juu ya uwepo wa chatu huyo ambaye amekuwa tishio kwa wakazi wanaofanya shughuli mbalimbali karibu na mto Meta.
Taarifa kutoka mkoani humo zinasema zoezi la kumtafuta nyoka huyo zilianza Jumatatu Mei 19, 2014 sikihusisha wataalamu wa Wanyamapori pamoja na waganga wa jadi ambao walikuwa wakimtafuta pembezoni mwa mto huo.
MBEYA
Tangazo lililotolewa na Halmashauri Mbeya
Juhudi hizo zilianza kuonyesha mwanga asubuhi ya Jumatano Mei 20, 2014 wakati waganga wa jadi walipofanikiwa kumpata chatu mdogo pembezoni mwa Mto Meta karibu na Hoteli ya Rift Valley.
Mganga wa jadi, Mazoea Hamis (39) mkazi wa Chalinze mkoa wa Pwani, alisema siku ya kwanza ya zoezi hilo walifanikiwa kugundua njia aliyokuwa amepita chatu huyo lakini hawakufanikiwa kumpata hadi jana walipofanikiwa kumpata chatu mdogo.
“Jioni yake baada ya kupumzika tuliona tuweke dawa za kienyeji ambazo zingiweza kumtoa mafichoni na kusogea karibu ambapo asubuhi jana tuliwahi kufika katika eneo hilo na kuendelea kumtafuta na bado tunaendelea kumtafuta” alisema Hamis.
Mbeya 1Eneo lenye msitu unaodaiwa kuwa umehifadhi nyoka mkubwa aina ya Chatu ambaye anatishia wakazi wa jiji hilo
Alisema baada ya muda wakati wakiendelea kufyeka kichaka chenye majani, mmoja wao alimkanyaga chatu huyo na yeye kukurupuka ndipo alipofanikiwa kumkamata. Mganga huyo ambaye anasaidiwa na, Athman Keneth (30), mkazi wa Chunya mkoani humo, alisema Chatu waliyemkamata ni mdogo na hivyo juhudi za kuendelea kumtafuta Chatu mkubwa zitaendelea kama kweli yupo au ametoweka ili kuondoa hofu iliyopo.
Mbeya-SHIKA NYOKA WAGANGA
Mganga wa jadi, Mazoea Hamis (39) mkazi wa Chalinze mkoa wa Pwani aliyevalia nguo nyekundu zote, akiwa na Athman Keneth (30), mkazi wa Chunya mkoani humo ambaye anamsaidia ili kumpata chatu huyo
Alisema kwa kawaida chatu mdogo anapoonekana, mkubwa anakuwa anahama ili kuwapisha wadogo kuendelea na maisha yao au kwa namna moja au nyingine kusombwa na maji katika kipindi cha mvua kutoka kwenye hifadhi zao pamoja na wengine
Taarifa kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Jiji zinadai kuwa, baada ya kukamatwa kwa chatu huyo atahifadhiwa na kutunzwa katika Hifadhi ya Wanyama ya Ifisi ambako kuna wanyamapori wengine kwa ajili ya maonyesho.

MJUMBE Sr

About Author

Advertisement

Post a Comment

 
Top