Kikosi cha Mbeya City
Kikosi cha Mbeya City
Baada ya kupigwa danadana na kujawa na sintofahamu juu ya ushiriki wao katika mashindano ya mto nile hatimaye safari ya Mbeya City FC kwenda kushiriki michuano hiyo mipya ya CECAFA Nile Basin Cup nchini Sudan imekamilika baada ya kutumiwa tiketi za ndege.
Kocha msaidizi wa klabu hiyo Maka Mwalyisyi amesema kuwa wamepokea tiketi na wanaanza safari alfajiri ya kuamkia kesho na wanatarajia kufika Sudan kesho ijumaa majira ya saa 11:00 asubuhi kwa saa za huko.
Mwalwisyi amesema kwa mujibu wa Ratiba wanatakiwa kushuka dimbani kesho dhidi ya El Mereikh ya Sudan, lakini wapo katika mazungumzo ya kuomba kubadilishiwa ratiba kwasababu watakuwa wamechoka na safari.
“Tulitakiwa kucheza kesho. Lakini kuna mazungumzo yanaendelea ili kubadilishia ratiba. Kila kitu kinakwenda sawa na muda si mrefu tutaeleza kitakachojiri”.Amesema Mwalwisyi.
Hata hivyo, Mwalwisyi amesema wachezaji wote wapo katika hali nzuri na wamefurahi kuona safari imekamilika.
MJUMBE Sr