Kama kuna kitendoa ambacho kimewashtua, kuwasikitisha na kuwaumiza
Watanzania wengi wiki hii ni habari ya mtoto ambaye inadaiwa alikuwa
anaishi kwenye boksi tangu akiwa mdogo sana na kumsababishia madhara
makubwa ya kimaumbile na hatimaye kumsababishia kifo. Mtoto huyu Nasra
Rashid amegusa mioyo ya watu wengi lakini pia ametufanya tujiulize
maswali mengi kuhusu Mama Mlezi (dada wa marehemu mamake) lakini pia
zaidi kuhusiana na Babake mzazi ambaye alijitokeza baadaye (pichani mama
mlezi na babake mzazi). Majirani ndio inasemekana walilifichua jambo
hili lakini inaonekana walikuwa wanajua uwepo wa mtoto huyu kwa muda
mrefu.
Je, kama wewe ungeona mtoto anatendewa hivi ungechukua hatua gani? Je,
umewahi kuona mtoto anatendewa vibaya na ukaingilia kati? Au tunaonekana
tumeguswa kwa sababu mtoto amekufa?
Tafakuri:Mali ya Mimi Mwanakijiji
MJUMBE Sr
Post a Comment