Unknown Unknown Author
Title: JULIANA SHONZA AFICHUA SIRI;AMTAKA MCHUNGAJI MSIGWA AANZE KUFUNGASHA VILAGO VYAKE!!
Author: Unknown
Rating 5 of 5 Des:
Na MatukiodaimaBlog ALIYEKUWA  kada maarufu  wa chama cha Demokrasia na maendeleo (Chadema ) Taifa Juliana Shonza ambae alijiuzulu na cha...

Na MatukiodaimaBlog

ALIYEKUWA  kada maarufu  wa chama cha Demokrasia na maendeleo (Chadema ) Taifa Juliana Shonza ambae alijiuzulu na chama hicho na kijiunga na CCM amewataka wakazi wa jimbo la Iringa mjini kuungana kulipokea jimbo kutoka kwa mbunge Mch Peter Msigwa.

Shonza ametoa kauli hiyo leo wakati akiwahutubia wakazi wa jimbo la Iringa mjini wakati wa mkutano wa uzinduzi wa matawi unaofanywa na katibu mkuu wa Uvccm Taifa sixtus Mapunda.

Alisema jimbo la Iringa mjini ni jimbo ambalo wananchi walichagua mbunge kwa hasira na kuwa badala ya kutegemea maendeleo wamejikuta wakifanya maandamano yasiyo na kikomo kila uchwao.

Shonza alisema kuwa mbunge wa jimbo la Iringa mjini amekuwa ni mtu wa kujipigania mwenyewe kimaisha badala ya kujishughulisha kuwaletea wananchi maendeleo.

Hivyo alisema ni vema wananchi wa Iringa mjini kujipanga kwa hafla ya kulipokea jimbo hilo kutoka kwa mpangaji mbunge Msigwa aliyepanga bila kujua kama kapangishwa hivyo kushindwa kulipa kodi.

Akielezea juu ya hofu ya muungano wa vyama vinavyounda katiba ya wananchi (ukawa) alisema kuwa Chadema ni chama ambachokinataka kupanda kupitia ukawa.

Kwani alisema Chadema ndio chama kilichokituhumu CUF kuwa ni CCM  B na kuwa ni chama cha kishoga imekuwa leo kuungana 

Hivyo kuwataka watanzania kupima na kutoa maamuzi magumu pindi uchaguzi utakapo fika.

Nae mjumbe wa kamati ya utekelezaji Uvccm Taifa Secky Kasuga alisema wananchi wa jimbo la Iringa walianzimisha jimbo hilo na sasa mwenye Nyumba anahitaji Nyumba Yake hivyo lazima mpangaji kuondoka.

"Tunalazimika kuchukua Nyumba yetu baada ya mpangaji kushindwa kufagia nyumba"

Katibu mkuu wa UVccm Taifa Sixtus Mapunda alisema kilio cha maendeleo kwa jimbo la Iringa kimetokana na mchanganyo uliofanywa na wananchi kwa kumchagua mbunge mrudisha nyuma maendeleo.

Alisema mbunge amekuwa kikwazo kikubwa kwani bungeni wakati wa vikao vya bajeti yeye anatoka nje ya bunge na wakati wa vikao vya kupanga shughuli za maendeleo halmashauri yeye anashiriki kuita maandamano.

" Tunawaombeni wana Iringa mtusaidie kurejesha jimbo kwa kumtoa mbunge mpinga maendeleo katika jimbo la Iringa mjini ambalo maendeleo yanaletwa kwa nguvu na ccm"

Bw Mapunda asema anawashangaa wapinzani kwa kuikataa katibu inayopendekezwa ambayo unazungumzia pia Haki ya kuishi hivyo  kupinga Kwao wanapinga hadi haki ya wao kuishi.

Alisema kuwa hoja Yao ni kutaka serikali tatu na si vinginevyo na kuwa wananchi lazima wapigie kura ya ndio katiba hiyo na pindi muda wa serikali tatu utakapofika basi itafanyika hivyo na si sasa.

Kuwa kuutaka utanganyika ni kuutaka ukoloni hivyo lazima kujitambua kuwa wakati wa kuongozwa na wakaloni umepita.
Credit:matukioDaima


#Je Unatamani Kumiliki Blog yako??
Wasiriana Nasi!!


MJUMBE BLOG
Ni Ukurasa wa Habari,Picha,Matukio,Matangazo.

#KUJERUHI hisia za watu/mtu si Kusudi letu.
MAONI PIGA:0752025002

About Author

Advertisement

Post a Comment

 
Top