Farid Musa ameongezewa wiki moja nyingine ya majaribio na Club Deportive Tenerife ya nchini Hispania ambako ameenda kusaka mafanikio ya soka la kulipwa nje ya Tanzania.
Yusuf Bakhresa ambaye yuko pamoja na Farid nchini Hispania, ameiambia www.shaffihdauda.co.tz kwamba inavyoonekana mpaka sasa Farid ananafasi kubwa ya kubaki kwenye klabu hiyo.
Winga mshambuliaji wa timu ya taifa ya Tanzania na Azam FC Farid Musa yupo Hispaniaanaendelea na majaribio yake ya kutafuta nafasi ya kucheza soka la kulipwa,Farid ameendelea na majaribio yake Club Deportive Tenerife ya Hispania.
Farid amethibitisha kuendelea vizuri kiafya lakini amekaririwa na vyombo vya habari kuwa ana siku ya nne Club Deportive Tenerife ambapo hapo anakaa wiki moja halafu anaendelea na majaribio katika vilabu vingine vya hapo Hispania alivyotafutiwa na wakala wake John Sorzano
Credit:Shaffih Dauda




Post a Comment