NDOA YA NASSARI, HALIMA MDEE YAOTA MBAWA, JAMAA ANAOA KESHO!
Joshua Nassari na Halima Mdee, mwaka 2012
Na Mwandishi wa brotherdanny5.blogspot, Meru
UWEZEKANO
wa kuwepo kwa ndoa baina ya mbunge kijana wa Chadema wa jimbo la
Arumeru Mashariki, Joshua Nassari, na Mbunge wa Jimbo la Kawe (Chadema),
Halima Mdee, umeota mbawa baada ya taarifa kubainisha kwamba Nassari
sasa anatarajia 'kuvuta' jiko kesho katika kanisa moja huko Arumeru.
Mdada
ambaye ameuvutia moyo wa Nassari ametajwa kwa jina na Anande Nko, na
kwamba jana ndiyo ilikuwa 'Send Off' yake tayari kwa tukio kubwa la
harusi.
Mahaba
baina ya Nassari na Halima Mdee yalidaiwa kuchomoza mwaka 2012 wakati
ule mbunge huyo akiwa ameteuliwa kuwania ubunge katika uchaguzi mdogo
kufuatia kifo cha mbunge wa jimbo hilo, Jeremiah Solomon Sumari, ambaye
pia alikuwa naibu waziri wa fedha.
Wakati
wa kampeni zake, taarifa zilizagaa kwamba moyo wa Nassari ulikuwa
umemdondokea Mdee na yeye mwenyewe hakuweza kulificha hilo.
Nassari
alitangaza ndoa yake na Halima Mdee katika kipindi chote cha kampeni na
hata baada ya uchaguzi mdogo wa ubunge wa jimbo lake mwezi Aprili mwaka
2012.
Wachunguzi
wa masuala ya siasa mkoani hapa wanasema hii pia ni mbinu mojawapo ya
kujiandaa na kinyang’anyiro cha kutetea nafasi yake kwenye uchaguzi mkuu
ujao wa mwaka 2015.
Katika
uchaguzi uliopita, Nassari alipata shida kubwa sana kutoka kwa
wapinzani wake waliodai kuwa kwa sababu ni kapera isingekuwa jambo la
busara kwa wananchi wa jimbo hilo kumchagua.
Hatua
hiyo ilisababisha mbunge huyo kuamua kumtangaza hadharani Mdee kama
mchumba wake ambaye wangefunga naye ndoa mara tu baada ya kumalizika
uchaguzi mdogo wa jimbo hilo.
Hata
baada ya ushindi wake, Nassari aliendelea kumnadi Halima Mdee kuwa ni
mkewe mtarajiwa na anatarajia kufunga ndoa kubwa sana ambayo nayo
ingeweza kuhudhuriwa na viongozi wa kitaifa kutoka ndani na hata nje ya
Chadema.
Lakini
baada ya uchaguzi huo mdogo kupita bado Nassari hakuweza kuizungumzia
ndoa hiyo hali ambayo ilifanya wananchi wa jimbo hilo kubaki na
mshangao.
Jitiada
za kumpata mbunge azungumzie suala hilo ziligonga mwamba blogu hii
kuwasiliana kupitia simu yake ya kiganjani na yeye kusema kwamba yuko
kwenye kikao.
Aidha, blogu hii ilimtafuta Halima Mdee, lakini simu yake ya kiganjani haikuweza kupatikana.
Hii hapa ni habari iliyopamba magazeti Aprili 16, 2012:
MBUNGE
wa Kawe, Halima Mdee (Chadema) amesema sasa yuko tayari kufunga ndoa na
Mbunge mteule wa chama hicho wa Jimbo la Arumeru Mashariki, Joshua
Nassari.
“Nafurahi
kwamba Nassari hatimaye ameshinda ubunge katika uchaguzi mdogo,”
alisema Mdee wakati akihutubia maelfu ya wakazi wa Arusha na Meru juzi
katika viwanja vya Leganga kusherehekea ushindi wa chama chake katika
uchaguzi huo.
Mdee
alifafanua, kwamba yeye na chama chake walikuwa wamebanwa na kampeni za
kuhakikisha Chadema inatwaa jimbo la Arumeru Mashariki na ndiyo sababu
hakujibu mara moja maombi ya Nassari ya kumwoa aliyoyatoa katika moja ya
mikutano yake ya kampeni.
“Naondoka
kwenda Dar es Salaam kujiandaa kwa Mkutano ujao wa Bunge, kisha
nitakwenda Dodoma ambako nitamsubiri Nassari na kwa pamoja tutafanya
maandalizi,” alisema Mdee huku akishangiliwa na hadhira hiyo huku
wakiimba na kucheza katikati ya mvua iliyokuwa ikinyesha.
Mdee alisema ndoa kati ya wabunge hao wawili wa Chadema ni wazo zuri na itatangazwa sana na kuandika historia.
Alipoona
anashambuliwa sana na wapinzani wake juu ya useja wake katika kampeni
hizo, Nassari hatimaye alitangaza kumwoa Mdee ambaye pia hajaolewa.
Na katika moja ya mikutano ya hadhara, alisimama naye jukwaani kukampeni.
“Kuna
viongozi wengi wa kidini Dodoma, ikiwa ni pamoja na ndani ya Bunge
ambao watatushauri jinsi ya kulitimiza hili,” alisema Mdee na kuongeza
kwamba baba yake Joshua, Mchungaji Samuel Nassari alipata kusema,
‘mwanamke mzuri ni zawadi kutoka kwa Mungu’.
Chadema
ina idadi kubwa ya wabunge vijana ambao hawajaoa, ikiwa ni pamoja na
Mbunge wa Mbeya Mjini, Joseph Mbilinyi ‘Mr Sugu’; wa Ubungo, John
Mnyika; wa Kigoma Kaskazini, Zitto Kabwe na sasa Nassari.
SOMA ZAIDI.....
Na Dixon Busagaga wa globu ya jamii kanda ya kaskazini.
MBUNGE wa Jimbo la Arumeru Mashariki ,Mh Joshua Nassari kesho anatarajia kufunga ndoa na Bi Anande Nko katika kanisa la Pentekoste, Kilinga lililoko wilaya ya Meru ambako Mh Nassari alianzia masuala ya Kiimani ikifuatiwa na Sherehe kubwa ya Harusi itakayo fanyika katika viwanja vya Usa-River Academy jirani na Hotel ya Ngurdoto.
"Nichukue tena fursa hii kuwakaribisha ndg, marafiki, Jamaa na zaidi sana wananchi wangu wa jimbo la Arumeru Mashariki kwenye tendo hadhimu la kusherekea harusi yangu , Jumamosi Juni 7, Usa-River academy grounds kuanzia saa saba mchana. Kwa Pamoja Tulianza na Mungu, Tutamaliza na Mungu Pamoja. ...No cards on entrance!"alisema Nassari.
SOMA ZAIDI.....
JOSHUA NASSARI (MB) KUFANYA HARUSI YA ALAIKI KESHO JIMBONI KWAKE
![]() |
| Askofu Mkuu wa Dayosisi ya Meru Dr Paul Akyoo akifanya maombi kwa Bw Joshua Nassari ,Mbunge wa jimbo la Arumeru Mashariki na Bi Anande Nnko wanaotarajia kufunga ndoa Jumamosi hii. |
![]() |
| Mbunge wa jimbo la Arumeru Mashariki ,Joshua Nassari akimwimbia mchumba wake Bi Anande Nnko wakati wa sherehe ya Send off iliyofanyika nyumbani kwao na Bi Harusi Mtarajiwa ,Meru. |
![]() |
| Bi ,Harusi Mtarajiwa Anande Nnko akimpatia zawadi ya T-Shirt Mumewe Mtarajiwa Bw Joshua Nassari wakati wa sherehe ya Send Off iliyofanyika nyumbani kwao Meru. |
Na Dixon Busagaga wa globu ya jamii kanda ya kaskazini.
MBUNGE wa Jimbo la Arumeru Mashariki ,Mh Joshua Nassari kesho anatarajia kufunga ndoa na Bi Anande Nko katika kanisa la Pentekoste, Kilinga lililoko wilaya ya Meru ambako Mh Nassari alianzia masuala ya Kiimani ikifuatiwa na Sherehe kubwa ya Harusi itakayo fanyika katika viwanja vya Usa-River Academy jirani na Hotel ya Ngurdoto.
Kwa Mujibu wa Mh Nassari
,sherehe hizo zitakazoanza majira ya saa saba mchana watu wote
wamealikwa wakiwemo ndugu, marafiki, Jamaa na wananchi jimbo la
Arumeru Mashariki kwenye tukio hilo na kamba hakuna
kadi.
"Nichukue tena fursa hii kuwakaribisha ndg, marafiki, Jamaa na zaidi sana wananchi wangu wa jimbo la Arumeru Mashariki kwenye tendo hadhimu la kusherekea harusi yangu , Jumamosi Juni 7, Usa-River academy grounds kuanzia saa saba mchana. Kwa Pamoja Tulianza na Mungu, Tutamaliza na Mungu Pamoja. ...No cards on entrance!"alisema Nassari.
Na ssari amesema watu zaidi
ya 8000 wanatazamiwa kushiriki katika sherehe hiyo ya aina yake
wakiwemo viongozi mbalimbali na wabunge kutoka maeneo mbalimbali
.
Na Michuzi Media Group
Na Michuzi Media Group
MJUMBE Sr





Post a Comment