Tukiwa bado kwenye headlines za Uchaguzi
2015 kuna taarifa ambazo zilikuwa zinasambaa hivi karibuni kwamba
Mahakama ya kimataifa ya ICC itakuja Tanzania kusimamia Uchaguzi.
Sasa leo ripota alikutana na Mkurugenzi wa huduma za kisheria wa tume ya
Uchaguzi, Emmanuel Kawishe kupata majibu sahihi kuhusiana na taarifa
hizo..‘Kawaida taasisi ili ije kutazama
uchaguzi lazima itume barua ya maombi lakini kwa ICC bado hawajaomba na
kuna category za taasisi zinataka kuomba kwa hiyo kama itaangukia
kwenye sifa basi tutaruhusu lakini kama hiyo taasisi haina sifa
haturuhusu, kwa sasa tumepokea taasisi za kimataifa kama 20 na za hapa
ndani ni zaidi ya 60’ – Emmanuel Kawishe
‘Kwa hiyo
tunaendelea kupokea na tunaendelea kuangalia taasisi zingine zinakosa
vigezo tunawaambia taasisi zenu hazijakizi vigezo nendeni halafu mrudi
tena kwa hiyo wale wanaokizi vigezo tunawapokea‘ – Emmanuel Kawishe
Credit:MilardAyo
Post a Comment