Hivi ndivyo Barabara ilivyokuwa kabla
Waandishi
wa Jiji wakiwa wamefika kuwashangaa wenzao wakiwa wanafanya kazi ya
kutejenga Taifa , wa pili kutoka kushoto ni Mwandishi wa Habari wa Bomba
Fm Radio Richard Kamanga aliyekuwa akifanya kazi ya kutengeneza
Barabara hiyo akiongea nao.
Baadhi
ya wamachinga na wananchi wa eneo hilo aibu zikiwa zimewashuka na
kuamua kushirikiana na Waandishi wa Habari kutoka Bomba Fm Radio na
Mbeya yetu Blog kuendelea kutengeneza njia hiyo
Waandishi wa Jiji wakiahidi kuleta kifusi kwa ajili ya kurekebisha Barabara hiyo
Wachina wakiwa wamefika eneo la tukio na kuahidi kuwa nao wataongeza nguvu katika ujenzi wa Barabara hiyo
Mchina akipata maelekezo juu ya Barabara hiyo
Wachina wakiwa wamefika eneo la tukio na kuahidi kuwa nao wataongeza nguvu katika ujenzi wa Barabara hiyo
Mchina akipata maelekezo juu ya Barabara hiyo
Hii ndio kazi kubwa inayoendelea kufanywa na Mbeya yetu Blog sambamba na Bomba Fm Radio .
Picha na Mbeya yetu
********************
Wakati
kazi ikiendelea baada ya Halmashauri ya Jiji la Mbeya kuingia Mitini,
na tukio hili kuripotiwa muda mchache uliopita kupitia Mtandao huu na
Bomba Fm Radio huku waandishi hao wakiendelea ya kujenga Taifa ndipo
Ghafla waandishi wa Halmashauri ya Jiji la Mbeya walipoweza kufika na
kuwashangaa wenzao wakiendelea kupiga kazi na baada ya kuona aibu
waliamua kuahidi kuleta kifusi kwa ajili ya matengenezo ya Barabara
hiyo.
Nao
Baadhi ya wamachinga wapenda maendeleo waliweza kujitokeza kwa ajili ya
kuwaunga mkono waandishi wa habari walioanzisha kazi hiyo na kuwasaidia
kazi inayo endelea ya ukarabati wa kipande hicho cha barabara.
Wachina nao hawakuwa mbali baada ya kusikia ripoti ya tukio hili wakaamua kufika kujionea wenyewe, na wao kuahidi kutoa mchango wao wa kuweza kutengeneza barabara hiyo.
Wachina nao hawakuwa mbali baada ya kusikia ripoti ya tukio hili wakaamua kufika kujionea wenyewe, na wao kuahidi kutoa mchango wao wa kuweza kutengeneza barabara hiyo.
MJUMBE Sr
Post a Comment