Unknown Unknown Author
Title: ALICHO KISEMA KUBENEA BAADA YA GAZETI LA MWANAHALISI KUFUNGULIWA!
Author: Unknown
Rating 5 of 5 Des:
Pichani ni Mkurugenzi wa Kampuni ya Hali halisi  Saed Kubenea akiyatambulisha matoleo ya Magazeti mwanahalisi yaliyosababisha Gazeti kufu...
Pichani ni Mkurugenzi wa Kampuni ya Hali halisi
 Saed Kubenea akiyatambulisha
matoleo ya Magazeti mwanahalisi yaliyosababisha Gazeti kufungiwa
picha na Maktaba



MAHAKAMA Kuu ya Tanzania imesema Waziri wa Habari, Dk. Fennela Mkangara hakufuata utaratibu wa kisheria katika kulifungia gazeti la MwanaHALISI Julai 30 miaka mitatu iliyopita. Anaandika Erasto Stanslaus … (endelea).
Jaji Salvatory Bongole amesema Sheria ya Magazeti ya mwaka 1976 aliyoitumia kufungia gazeti hilo lililokuwa linachapishwa kila Jumatano na kampuni ya Hali Halisi Publishers Ltd (HHPL), inaelekeza kuwa pamoja na hatua nyingine kutaka maelezo ya utetezi kwa mchapishaji.
Katika uamuzi wa shauri lililofunguliwa mara baada ya MwanaHALISI kufungiwa, Jaji Bongole amesema gazeti hilo liko huru kuchapishwa kuanzia sasa.
Jaji huyo amesema pamoja na uamuzi huo, kampuni iliyolalamika imepewa mafao yote iliyoyaomba katika kufungua shauri hilo la mapitio ya uamuzi wa Waziri – prerogative orders.
Miongoni mwa maombi ya faida ni HHPL kulipwa gharama za kesi pamoja na fidia kutokana na hasara iliyopatikana kwa muda wote wa gazti hilo kuwa kifungoni.(P.T)
Wakati Waziri alipofungia gazeti la MwanaHALISI, alieleza kwamba sababu ni kuandika habari na makala za uchochezi.
Habari hasa iliyoikera serikali hata kujilazimisha kuchukua hatua hiyo katili, ilikuwa ni iliyohusu uchunguzi wa tukio la kutekwa na kuteswa hadi karibu na kifo kwa aliyekuwa Mwenyekiti wa Chama cha Madaktari Tanzania (TMA), Dk. Steven Ulimboka.
Dk. Ulimboka alikumbwa na mkasa huo mnamo Juni 2012 alipotekwa usiku eneo la Tazara, karibu na viwanja vya Leaders Club, Kinondoni, ambako aliitwa na mtu aliyemtaja kuwa ni ofisa wa Ofisi ya Waziri Mkuu, ambaye alikuwa na mawasiliano ya karibu naye kwa saa kadhaa siku chache na usiku huo siku yatukio.
Daktari huyo aliyekuwa mtumishi wa taasisi ya Marekani nchini, alifika eneo la Tazara akifuatana na daktari mwenzake aitwaye Deo, ambaye mara baada ya tukio hilo, wakati wa alfajiri, alimpigia simu Mhariri wa MwanaHALISI, Jabir Idrissa, kumjulisha kuhusu kutekwa kwa Dk. Ulimboka.
Kufuatia habari za kuachiwa huru kwa MwanaHALISI, Mhariri huyo amesema amefurahishwa na uamuzi wa mahakama ya Tanzania, kwa kuwa umethibitisha kosa la serikali la kujichukulia maamuzi mkononi chini ya kuvunja sheria ilizoahidi kuzilinda.
“NImefurahi sana kuthibitishiwa kwamba serikali ilikosea katika kufungia gazeti. Uamuzi wa jaji umesema waziri hakufuata hatua za kisheria alizopaswa kuchukua kabla ya kufungia gazeti, ikiwemo ya kuwapa wamiliki na mhariri nafasi ya kujitetea,” amsema Idrissa.
“Lakini pia uamuzi huu unatakiwa uwe funzo muhimu kwa utawala kwamba hauwezi kudumu na kudumu kwa msisitizo wa kuhifadhi na kufurahia sheria zilizopitwa na wakati ambazo miaka kadhaa nyuma zilishatangazwa kuwa ni sheria kandamizi,” alisema.
Mhariri amesema anawasiliana na mmiliki na mchapishaji wa MwanaHALISI, kampuni ya HHPL, kukamilisha taratibu za kuchapisha toleo la kwanza haraka iwezekanavyo. Gazeti hilo lilikuwa likichapishwa mara moja kwa wiki siku ya Jumatano.
Kwa muda wote ambao gazeti hilo linatumikia kifungo, viongozi waandamizi serikalini, akiwemo rais Jakaya Kikwete, wamekuwa wakitamba kuwa hawatavumilia gazeti linalochapisha habari za uchochezi.

SOMA ZAIDI:
HATIMAYE  Mahakama kuu imelifungua rasmi Gazeti la Mwanahalisi ambalo lilifungiwa na serikali kwa mda usiojulikana .Anaandika KAROLI VINSENT endelea nayo.
       Akizungumza na Fullhabari.blogs, Mhariri wa Gazeti la Mwanahalisi ,Jabir Idrisa amethitisha kuwa Jaji wa mahakama kuu Salvatory Bongole,amelifungulia Gazeti hilo na kulitaka liendelee na kazi yake ya kuhabarisha umma  baada kubainika katika kulifungia kwake kanuni zilikiukwa.
        Amesema hukumu hiyo imetokana na kesi namba 27 ya mwaka 2013 ambapo Kampuni ya Hali halisi limited  ambao ni wachapishaji wa Gazeti la Mwanahalisi walikuwa wakitaka patio la hatua ya waziri wa Habari Fenera Mukangala juu ya kulifungia  Gazeti hilo, Katika kesi ambayo iliwakilisha kwa  Upande wa Serikali  na ofisi ya Mwanahseria mkuu  wa Serikali
Jabir amesema Mahakama imebaini waziri wa Habari hakufuata  sheria katika kulifungia gazeti hilo,licha ya kuwa na mamlaka ya kutokana na sheria ya Kandamizi ya  Magazeti ya mwaka 1976 inampa  uwezo wa kulifungia gazeti,
    Amesema Sheria iyo inamtaka waziri husika kufuata hatua kabla ya kulifungia Gazeti ambapo hatua hiyo ni kuwafuata wale anawaowatuhumu ili wapate utetezi na kuchukua hatua lakini waziri huyo alipolifungia Gazeti hilo  hakufuata hatua hizo.
   HATUA GANI INAFUATA BAADA YA HUKUMU HIYO.
Mwandishi huyo mwandamizi amesema kwa sasa kinachofuata ni kutaka fidia toka serikalini juu ya hasara iliyopatika wakati Gazeti hilo lilipokuwa limefungiwa huku akisema mahakama imeamulu wafanye hivyo.
      Amesema Chengine kinachofuata  ni mwenyewe Mmiliki wa Gazeti hilo akiamua kuchapisha Gazeti hilo  anachapisha  au aache kutokana na mahakama hiyo kumruhusu.

Kufunguliwa huko kwa Gazeti la kiuchunguzi la Mwanahalisi kunakuwa ni kama ushindi kwa Mkurugenzi wa Gazeti Saed Kubenea Mara kwa mara amekuwa ikidai serikali kulifungulia Gazeti hilo kimakosa……………………………

About Author

Advertisement

Post a Comment

 
Top