Unknown Unknown Author
Title: ALICHO KISEMA MJENGWA NA HULKA YA USHABIKI....!
Author: Unknown
Rating 5 of 5 Des:
...



 
Njau, Kalumekenge Na Ushahidi Wenye Utata!

Ndugu zangu,
Kuna kisa cha hakimu aliyepata tabu sana katika kuthibitisha ukweli wa urefu wa mtuhumiwa wa wizi. Mashahidi walikuwa wawili; Njau na Kalumekenge.
Wote wawili, Njau na Kalumekenge, walimwona mtuhumiwa akivunja mlango wa nyumba kabla ya kuingia ndani na kuiba.
Utata wa ushahidi wao ni kuwa; shahidi Njau alitamka kwa kujiamini mahakamani kuwa mwizi alikuwa mfupi. Na shahidi Kalumekenge naye aliongea kwa kujiamini kuwa mwizi alikuwa mrefu.
Huu ni ushahidi wenye utata uliopelekea Bwana Hakimu aumize kichwa kabla hajapata njia ya kutatua utata huo.
Hatimaye , hakimu akapata njia ya kufahamu urefu halisi wa mtuhumiwa wa wizi. Ndio, hakimu alibaini, kuwa kwa vile shahidi Njau ni mrefu, yeye alimwona mwizi kuwa ni mfupi. Na kwa vile shahidi Kalumekenge ni mfupi, kwake mwizi huyo alikuwa ni mrefu.
Basi, Bwana Hakimu alichofanya ni kutafuta wastani wa urefu wa Njau na Kalumekenge ili kupata urefu halisi wa mtuhumiwa wa wizi ambaye Njau na Kalumekenge walimwona kwa wakati mmoja.
Kuna tunachojifunza katika utata na utatuzi wa ushahidi huo. Umuhimu wa mwanadamu kutokuwa na hulka ya kukurupuka na kuamua mambo. Kuacha ushabiki. Umuhimu wa kutafakari kwa kina kabla ya kuamua.
Maana, duniani hapa aliye juu anaweza kuyaona mambo kwa mtazamo wake, na aliye chini vivyo hivyo. Kwamba wanadamu tunayoyaona tunayaona kwa mitazamo tofauti. Vivyo hivyo kwa tunayoyasikia na kuyaangalia. Kwamba wanadamu tuna hulka ya kusikia tunachotaka kusikia, na kuona tunachotaka kuona. Na mjinga asipojua kuwa yeye ni mjinga unafanyaje?
Ni Neno Fupi La Usiku.
Maggid

About Author

Advertisement

Post a Comment

 
Top