Unknown Unknown Author
Title: BENK YA WANA WAKE TANZANIA WAMEFUNGUA OFISI IRINGA
Author: Unknown
Rating 5 of 5 Des:
Na Said Ng'amilo Iringa. Wanawake na vijana wametakiwa kujiunga katika vikundi vya kiuchumi na hatimaye kupat...
DSC_0182_9d49a.png
Na Said Ng'amilo
Iringa. Wanawake na vijana wametakiwa kujiunga katika vikundi vya kiuchumi na hatimaye kupata mikopo yenye masharti nafuu kwa ajili ya kuanzisha na kuendesha biashara kutoka Benki ya Wanawake (TWB).
Akizungumza na Waandishi wa habari mjini hapa, Mkuu wa Shughuli za utendaji na maendeleo ya Benki, Yebete Zabron alisema vijana wengi wanapomaliza vyuo wana mtizamo wa kuajiliwa jambo ambalo limepitwa na wakati kutokana na ugumu wa kupata ajira zenyewe na mabadiliko ya kiuchumi duniani.
Alisema jambo la msingi ni kujiunga katika vikundi vidogo vidogo vya kiuchumi, kupatiwa mafunzo ya jinsi ya kuanzisha na kuendesha biashara na haatimaye kupata mikopo yenye masharti nafuu.
Alisema jamii inatakiwa kuachana na mazoea ya kwenda kukopa mitaani kwa riba kubwa wakati kuna taasisi za kifedha kama benki hiyo ambazo zinatoa mikopo yenye masharti nafuu na kwa riba ndogo ikilinganishwa na ile inayotozwa kwenye vikundi vilivyo nje ya mfumo rasmi.
Zabron alisema lengo la benki hiyo ni kuwainua wanawake kiuchumi kwa sababu wamekuwa nyuma katika familia licha ya kuwa na umuhimu katika ustawi wa familia na jamii kwa ujumla.
Alisema pia kwa hapo baadaye wataanza kutoa mikopo ya bodaboda na bajaji ili kuwasaidia vijana wengi kuingia kwenye biashara hiyo na kuongeza vipato vyao.
Alisema hivi karibuni watafungua huduma ya benki wakala ambapo wataweza kutoa huduma zote za kibenki kupitia mawakala hao ambao watakuwepo katika kila wilaya na kila ilipo ofisi ya Posta lengo likiwa kuafikia wenye kipato cha chini wote.
Hata hivyo alitahadharisha kuwa ni vema mikopo ambayo wanawake na vijana watachukua waitumie vyema na si kwa ajili ya kuongeza nyumba ndogo na kufanya starehe bali ilenge kufanya maendeleo ya familia.
Afisa mikopo Msimamizi wa Iringa, Baker Gunje alisema mteja wao hafungwi kurejesha mkopo haraka na kuweza kupata mkopo mwingine na kwa kufanya hivyo riba yake itapunguana kuwa wanatoa mikopo ya kuanzia Sh200,000 hadi 2,000,000.
Mkuu wa Shughuli za Kibenki na Maendeleo ya biasharaYebete Zablon akongea na waandishi wa Habari Mkoani Iringa kuhusu adhima ya TWB kufika mkoani hapo na kuanza shughuli zake za utoaji mikopo yenye asilimia ndogo kwa wafanyabiashara wadogo na wajinsia zote wa Iringa. 
(Picha na Said Ng'amilo)
(Martha Magessa)

MJUMBE Sr

About Author

Advertisement

Post a Comment

 
Top