Hali ya
wasi wasi imetanda huko Mombasa kufuatia kifo cha Sheikh Abubakar
Shariff Ahmed, maarufu kwa jina la Makaburi aliyewekewa vikwazo na
Marekani na Umoja wa mataifa kwa msimamo wake wa kuunga mkono kundi la
Al-Shabab, pamoja na kuwaandikisha vijana kujiunga na kundi hilo.
makaburi amekuwa akikanusha tuhuma hizo
.
Polisi
inaeleza kwamba mauaji hayo yaliofanywa na watu wasiojulikana wenye
silaha yametokea baada ya serikali ya Kenya kutangaza kwamba imeanza
operesheni ya kuzuia wimbi la mashumbilizi nchini humo, na kwamba
maafisa wa polisi wamewakamata zaidi ya watu 650 huko Nairobi kufuatia
milipuko mitatu ya bomu mjini Nairobi siku ya Jumatatu.
Ripoti ya kuuliwa kwa Sheikh Abubaker Ahmed -'Makaburi'
Ripoti ya kuuliwa kwa Sheikh Abubaker Ahmed -'Makaburi'
Wakili wa
Imam Ahmed, Mbugua Murithi amesema Sheikh Ahmed aliuwawa pamoja na mtu
mwingine asiyejulikana karibu na jela ya Shimo la Tewa nje ya mji wa
Mombasa.
Akizungumza
na Sauti ya Amerika Amin Mwidau, mchambuzi wa masuala ya kisiasa mjini
Toronto Canada, anasema ni kitendo cha kusikitisha lakini anasema mauaji
hayo yanatishia kuleta ghasia za kulipiza kisasi.
Mwidau
anasema hatari iliyopo kutokana na mauwaji yake kuna uwezekano wa
wafuasi wake na watu wengi kuamini zaidi mawaidha yake kwamba waislamu
wa Pwani Kenya wanakandamizwa.
Makaburi ni Imam wa tatu kuuliwa Mombasa katika kipindi cha chini ya miezi 6.
chanzo:VOA
MJUMBE Sr
Post a Comment