Unknown Unknown Author
Title: KITILA MKUMBO:TUSIVUNJE NCHI TULIYO IJENGA KWA MIAKA 50
Author: Unknown
Rating 5 of 5 Des:
Tarehe 9 Februari 1967 ndugu yake Sultani wa mwisho wa Zanzibar Muhammed bib Abdallah alimwandikia barua aliyekuwa Rais wa Marekani wakati...
Tarehe 9 Februari 1967 ndugu yake Sultani wa mwisho wa Zanzibar Muhammed bib Abdallah alimwandikia barua aliyekuwa Rais wa Marekani wakati huo akiiomba Marekani kuingilia kati muungano wa Tanganyika na Zanzibar akidai kuwa muungano huo ulikuwa haramu kisheria. Aliitaka Marekani iingilie kati ili kurudisha uhuru wa Zanzibar. Hata hivyo Ikulu ya Marekani ilijibu barua hiyo kwa kusisitiza kuwa ilikuwa inaunga mkono na kuutambua kikamilifu Muungano wa Tanzania. Hili likawa pigo la mwisho la Sultan Seyyid Jemshi bin Abdallah aliyekuwa bado anatamani kurudi Zanzibar. (Chanzo: Kitabu cha Ali Shabaan Juma, Zanzibar hadi mwaka 2000).
Kuna sauti zimeanza kujitokeza za kuhoji uhalali wa muungano wetu. Hii sio mbaya kama nia na dhamira ni kurekebisha na kuibuka na muungano imara na madhubutu zaidi. Lakini tuangalie tusijekujikuta tunafanya kazi ya watu wengine kwa kujua au kutokujua. Mimi nadhani tunaweza kabisa kudai serikali tatu bila kukejeli muungano huu. Kwa maoni yangu sioni mantiki ya kuhoji uhalali wa muungano huu miaka 50 baadaye. Tungependa kuona pande zote mbili zenye kutaka serikali mbili na tatu zikilenga kuimarisha muungano huu ili nchi Tanzania iendelee kudumu na kuwa imara zaidi.
Msingi muhimu wa majadiliano uwe kuhakikisha kwamba hatuvunji nchi tuliyoijenga kwa miaka 50.
Chanzo:Kitila Mkumbo

MJUMBE Sr

About Author

Advertisement

Post a Comment

 
Top