Unknown Unknown Author
Title: MAREKANI YAIONYA URUSI KUHUSU UKRAINE
Author: Unknown
Rating 5 of 5 Des:
Marekani imeonyesha wasiwasi wake kuhusu kile ilichokitaja kama harakati za kundi fulani linalotaka kujitenga ambalo limekuwa ...


Marekani imeonyesha wasiwasi wake kuhusu kile ilichokitaja kama harakati za kundi fulani linalotaka kujitenga ambalo limekuwa likisaidiwa na Urusi kuchochea ghasia mashariki mwa Ukrain.
Kufuatia kutekwanyara kwa vituo vya polisi katika miji kadhaa ya mashariki mwa Ukrain ,waziri wa maswala ya kigeni nchini marekani John Kerry amesema kuwa mashambulizi hayo ya watu waliojihami na silaha za Urusi yalifanyika kwa mpangilio.
Katika mazungumzo yao ya simu na waziri wa maswala ya kigeni nchini Urusi Sergei Lavrov,Kerry ameitaka Urusi kusitisha mashambulizi kama hayo la sivyo ikabiliwe na vikwazo zaidi.
Urusi imeonya kuwa utumiaji wowote wa nguvu nchini Ukrain utahujumu harakati za kidiplomasia kumaliza mgogoro huo
Chanzo:BBC
Mjumbe Jr.

About Author

Advertisement

Post a Comment

 
Top