Rais wa Tanzania Jakaya Mrisho
Kikwete ameipongeza Timu ya Watoto wa Mitaani ya nchi hiyo kwa kutwaa
Kombe la Dunia huko Rio de Janeiro nchini Brazil.
Taarifa iliyotolewa na ikulu ya Tanzania imesema Rais Kikwete afurahishwa jinsi watoto hao walivyonyakua kombe hilo la dunia."Mmetuwakilisha vyema, ninawapongeza sana, pia mmewapa moyo watoto wengine wote wenye vipaji maalum lakini hawakubahatika kuwa na makazi rasmi, hongereni sana" Rais amesema.
Timu hiyo ya watoto wenye umri chini ya miaka 16 ilipangwa kundi la 2 ambapo pia zilikuwapo timu kutoka Nchi za Argentina, Nicaragua,Philippines na Burundi.
Chanzo:bbc
MJUMBE Sr
Post a Comment