TAARIFA KWA UMMA
UPOTOSHAJI UNAOTOLEWA DHIDI YA TIMU YETU KUELEKEA MCHEZO WA TAREHE 13/4/2014
Kwanza nachukua nafasi hii
kuwashukuru kwa dhati wapenzi wote wa mchezo wa mpira wa miguu na
wapenzi wa Mbeya City Fc popote pale walipo kwa kuiunga mkono timu yao
muda wote wa michezo ya ligi kuu inayoelekea ukingoni hivi sasa.Klabu
inathamini nafasi ya wapenzi na washabiki katika kujenga timu imara na
yenye ushindani kama walivyofanya kwa timu yetu.
Timu yetu ilianza ligi msimu huu
2013/2014 ikiwa na malengo ya kuchukua ubingwa au kuwa katika nafasi za
juu za ligi yetu.Hiyo ndiyo dhamila iliyokuwepo kwa viongozi,wachezaji
pamoja na benchi la ufundi.
Michezo miwili imesalia kwa timu
yetu kabla ligi kuu ya Vodacom kumalizika katika msimu huu
2013/2014.katika safari yetu ya ligi kuu kwa mara ya kwanza msimu huu,
changamoto nyingi za kiutawala na za kimtazamo kutoka kwa wadau wote
wanaohusika na mchezo wa mpira wa miguu nchini tumezishuhudia
.Changamoto hizo ni ikiwemo upangaji wa ratiba usiyokuwa na uwiano
mzuri,baadhi ya mechi kuamuliwa vibaya na waamuzi wa mchezo,wizi wa
mapato ya milangoni unaotokana na mfumo mbaya wa uuzaji wa
tiketi,uadilifu mdogo kwa baadhi ya viongozi wenye dhamana ya kusimamia
mpira katika ngazi zote n,k.
Kuelekea mchezo wetu wa tarehe
13/04/2014 dhidi ya AZAM FC kumezuka propaganda chafu na ambazo si
sahihi katika ukuzaji wa mpira hasa wa ligi ndogo kama ya Tanzania.
Nachukua nafasi hii kutoa ufafanuzi wa baadhi ya mambo ambayo yamekuwa
sehemu ya propaganda hizo:
1. Klabu
imehaidiwa kununuliwa basi na hivyo inajiandaa kutoa ushindi kwa kwa
timu ya AZAM Fc na kuwarahisishia mazingira ya Ubingwa.
Halmashauri ya jiji la Mbeya
limekuwa katika mchakato wa kutafuta na kununua basi kwa ajili ya
matumizi mbalimbali ya Halmashauri ikiwemo kutumiwa na timu zake (
Netiboli na Mpira wa miguu)ambazo zote zipo ligi kuu ya michezo husika
kwa kufuata sheria ya manunuzi ya Umma. Mchakato huo ulianza
halmashauriilipotangaza nia hiyo katika gazeti la “the guardian” la tarehe hiyo kwa tender tarehe 8/8/2013o.LGA/069/2013-2014/MCC/G/01 hii
ni baada ya Halmashauri kutenga bajeti ya fedha za makusanyo yake ya
ndani kwa mwaka wa fedha 2012/2013 na 2013/2014 ili kukidhi haja hiyo.
Tangazo hilo halikupata mzabuni
mwenye sifa za kufanya usambazaji wa basi hilo hivyo tangazo hilo
lilirudiwa tena tarehe 12/2/2014 katika gazeti la majira kwa Tender No.LGA/069/2013-2014/MCC/G/01 (Re-advitised), Mchakato na maandalizi ya ufunguaji wa ufanyaji wa tathmini wa zabuni hiyo unaendelea kwa mujibu wa sheria ya manunuzi ya Umma.
Pamoja na mchakato huo hapo juu,pia
klabu inaendelea na mazungumzo na wadau mbalimbali wenye nia ya kuwekeza
kwa udhamini wa bidhaa zao,moja ya maeneo ya udhamini ni pamoja na
ununuzi wa basi la wachezaji taratibu na makubaliano haya yatakapo
kamili umma wa wapenda mchezo wa mpira wa mguu utajulishwa.
Hivyo propaganda hiyo kuwa klabu imehongwa basi si za kweli na si sahii ila zina nia ya kuidhalilisha timu yetu.
Awadh Ibrahim
MJUMBE sr
Post a Comment