Title: UTURUKI KUSHIRIKI MIRADI YA UJENZI NCHINI
Author: Unknown
Rating 5 of 5
Des:
...
KAMPUNI tatu kutoka Uturuki zimeingia
nchini kwa lengo la kushiriki katika ujenzi kwenye miradi tofauti katika
maeneo mbalimbali.Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya KAYA ya Uturuki, Orhan
Babaoglu, alisema kukua kwa sekta ya ujenzi nchini ndicho kigezo
kilichowafanya wafungue ofisi zao. Akizungumza kwa niaba ya Kampuni ya
Bosandra Professional Co. Ltd , Babaoglu alimpongeza Waziri wa Ujenzi,
John Magufuli kwa kusimamia sekta hiyo hadi kampuni kutoka Uturuki
kufungua ofisi zao nchini.
"Tumekuwa tukifuatilia uendeshwaji na
ukuaji wa sekta ya ujenzi katika mataifa mbalimbali barani Afrika na
tumejiridhisha kuwa Tanzania ni nchi inayofanya vizuri katika upande
huo," alisema Babaoglu. Mwakilishi mwingine wa Kampuni ya
CEYTUN, Kursat Durak, alisema utendaji wa kampuni kutoka Uturuki
unafahamika duniani kote, hivyo ujio wao una lengo la kuamsha ushindani
wa ubora lakini pia kuona gharama za utekelezaji wa miradi hiyo
zinadhibitiwa kwa kuwa na washindani kutoka maeneo tofauti. Chanzo:Mjengwa
The part time Blogger love to blog on various categories like Web Development, SEO Guide, Tips and Tricks, Android Stuff, etc including Linux Hacking Tricks and tips. A Blogger Template Designer; designed many popular themes.
Post a Comment