Waziri wa Uchukuzi, Dk. Harrison Mwakyembe
Habari
zilizopatikana hivi punde kutoka bungeni Dodoma ni kwamba ndege
tatuzinazovinjari upende wa Tanzania katika Ziwa Nyasa ni za Tanzania
zilizokodiwa na Serukali ya Malawi kwa ajili ya utafiti wa kijiolojia.
Taarifa hiyo imetolewa ma Waziri wa Uchukuzi, Dk. Harrison Mwakyembe,
bungeni Dodoma asubuhi hii, baada ya Mbunge wa Ileje, Aliko Kibona
kuitaka Serikali kutoa taarifa sahihi juu ya suala hilo, kwani zimekuwa
zikiwatia hofu wananchi waishio mpakani na Malawi.
Amesema kuwa ndege hizo zimekodiwa kutoka Dodoma Tanzania na kwamba
zimepata vibali vyote kutoa Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania (TCAA).
Mwakyembe, amewapongeza Watanzania kwa kuwa na uharaka wa kutoa
taarifa kwenye vyombo vya dola kwa jambo lolote wanalolitia wasiwasi
kama hilo
Endelea Kutu Tembelea Mtandaoni kwa Kuandika Neno MJUMBE BLOG na Kuingia Hapo ili Kupata Habari Mpya Mara kwa Mara.
mjumbe sR

Post a Comment