Kutokana na sanaa ya Bongo kuvamiwa na wimbi la vijana walio funga turbo za njaa matumboni mwao! Ambao katika sanaa wanacho angalia na Pesa na Suala la Maadili kwao sio kitu.Tabia yao ya kuwa Tayari kujidharilisha ili wawe maarufu na wa andikwe ama wavute atention ya watu ime Amsha hisia za gwiji la Sanaa ya vichekesho Bwana Amri Athumani ama King Majuto Kama
Anavyo fahamika miongoni mwa wengi.
Amekaririwa akisema
"...hawa wavamizi Ukiangalia... ..Unaweza kutapika.. Sipendi na Wana udhi,kama vipi wajipange upya.."
Mambo wanayo fanya mengine ni ya kujidharirisha!
Ni hivi majuzi tu BASATA lime wafungia MISS UTALII kwa Muda Usio julikana kutokana na kuonekana kuendeleza Utamaduni ambao umeonekana kuwa kinyume na maadili ya jamii yetu.Dada zetu na wadogo zetu wamekuwa kama wana chuuzwa sokoni kupitia kivuli cha Sanaa.Walezi na Wazazi wengi wame kuwa wakilalamika lakini kutokana na Nguvu ya mfumo pesa na Matangazo mengi ya kilaghai yanayo dhaminiwa na waovu hao Tumejikuta kama jamii tume jirahisi kiasi cha Kuupa kisogo Utamaduni wetu na maadili yetu.
Mimi nina Amini kuwa 'Utupu wa dada zetu ni utupu wa taifa letu lijalo'.
Elasto Mbella
Mjumbe
Mbeya
Post a Comment