MADUKA YAFUNGWA MWANZA KUPINGA MASHINE ZA TRA!
Wafanyabiashara jijini mwanza hapo jana walifunga maduka yao,kupinga kutumia mashine za kielektroniki(EFD) za mamlaka yamapato Tanzania(TRA),Zinazo tumika Kutoa Risti wakati wa bidhaa zao.
Wafanyabiashara hao waliamua kutofungua maduka yao wakipinga kulaimishwa kununua mashine wanazo dai zinauzwa kwa bei kubwa kati ya Tsh.600,000 na 800000.Mbali na kufunga maduka yao,wafanyabishara walipanga kuandamana kwenda katika ofisi za mamlaka ya mapato majira ya saa mbili asubuhi;Lakini maandano yao yalizuiliwa na polisi.Ulinzi uliimarishwa jijini kuhakikisha hakuna mikusanyiko yoyote ya makundi ya watu.
Meneja TRA mkoa wa Mwanza Jeremiah Lusana alisema mashine hizo lazima zinunuliwe na wafabiashara ili kuepuka kupoteza muda na Mapato.
MMJUMBE sr
22088348937962


Post a Comment