
Ndugu zangu,
Kesho
vumbi la kampeni litaanza kutimka rasmi. Kwa uzoefu wangu wa kufuatilia
siasa za nchi hii naziona ishara za yatakayotokea. Kwanza kutakuwa na
hali mbili zitakazojitokeza; Uhalisia na tamthilia. Kwamba mengine
yatakuwa ni maigizo ya kisiasa. Ni bahati mbaya pia, kuwa tutarajie
kushuhudia pia ushabiki wa kisiasa kwa mwenye kushabikia kushindwa
kuuona uhalisia. Ni kwenye kutanguliza ushabiki ndipo mtu hupenda
kusikia anachotaka kusikia, kuona anachotaka kuona. Ni vema na ni busara
kwa mwanadamu, kuwa na ujasiri pia wa kusikia usichopenda kusikia, na
kuona usichopenda kuona.
Mimi nitajitahidi kuyaangalia ya uhalisia. Ningependa msomaji nikusaidie pia kuyaona hayo ya uhalisia.
Ni uhalisia ninavyoandika sasa, kuwa CCM ina wakati mgumu kisiasa kuliko wakati mwingine wowote katika historia ya uwepo wake.
Ni katika
mazingira hayo, kuwa tutarajie, kuwa CCM itatumia nguvu ya chama chake
kumsaidia kumnadi mgombea wake ambaye wana hakika atakubalika. Hivyo,
kesho CCM hawatawatuma mgambo Jangwani kwenye uzinduzi wa kampeni zao;
CCM watakwenda na makamanda wao. Tutarajie pia, kuwa hata wale wenye
imani na CCM na ambao kwa kawaida huwa hawaendi kwenye mikutano ya CCM,
kuwa kesho wengi wao hawatakaa kwenye mikeka au makochi yao majumbani
wakiangalia runinga. Watainuka kwenda Jangwani kukipa sapoti chama chao.(P.T)
Ndio,
mkutano wa kesho wa CCM Jangwani utatoa ishara za itakavyokuwa baada ya
Oktoba 25. Na CCM ina historia ya kuendesha mikakati yake kwa kufuata
mbinu za kijeshi. Walio kwenye ' War Room' ndani ya CCM, kesho ndio
nafasi yao ya kuonyesha walivyojipanga. Kwa CCM, Mkutano wa Jangwani
kesho ni ' Mama Wa Mikutano Yote Ya Kampeni'.
Maana,
kihistoria, Dar es Salaam na muitikio wa Watu wa Dar es Salaam kujaa
Viwanja vya Jangwani imekuwa ni kipimo cha namna chama kinavyokubalika.
Hivyo, hatma ya Uchaguzi wa Mwaka huu inaweza kuamuliwa Jangwani.
Na baada ya hapo ni vita ya kwenye media kwa pande zote mbili. Atakayejipanga vema ana nafasi ya kuzoa kura nyingi pia.
Vinginevyo,
uhalisia mwingine ni kuwa, kama ilivyo Kwa wavuvi, kuna mtego wa samaki
unaitwa mgono. Ni aina ya tenga. Ni kubwa, pa kuingilia ni papana sana.
Samaki anaweza kuingia kwenye mgono bila kujua kuwa anaogelea kwenye
mgono. Hatimaye atafika mwisho na kuukuta upenyo mdogo.
Akivuka hapo samaki anaukuta mgono mwingine ndani ya mgono aliouacha nyuma yake. Na samaki akiogelea akafika mwisho, basi, mgono huo huwa umefungwa. Samaki hao watakuwa wameingia kwa wingi ndani ya mgono.
Na tabu ya samaki huwa hawana uwezo wa kuogelea kinyumenyume, na kwa kufuata utaratibu. Hivyo, samaki hao wote watakuwa wamenaswa kwenye mgono.
Akivuka hapo samaki anaukuta mgono mwingine ndani ya mgono aliouacha nyuma yake. Na samaki akiogelea akafika mwisho, basi, mgono huo huwa umefungwa. Samaki hao watakuwa wameingia kwa wingi ndani ya mgono.
Na tabu ya samaki huwa hawana uwezo wa kuogelea kinyumenyume, na kwa kufuata utaratibu. Hivyo, samaki hao wote watakuwa wamenaswa kwenye mgono.
Kama
mchambuzi wa habari na ninayefuatilia kwa karibu siasa za nchi hii,
naliona kosa kubwa la wapinzani kuiga hata makosa yanayofanywa na CCM na
hivyo wapinzani hao kujikuta wanaingia kwenye mtego wa mgono. Tunaona
vita ya kugombania baadhi ya majimbo. Lakini, huko chini kabisa,
wapinzani hawakupaswa kukaa Dar es Salaam na kuwachagulia wapiga kura
madiwani wa kusiamama kwenye chaguzi.
Wapinzani
walipaswa kujua, kuwa CCM bado ni chama chenye nguvu hata hii leo. Na
uhalisia ni kuwa, hata kama Uchaguzi Mkuu ungefanyika kesho Jumapili,
basi, CCM ndicho chama ambacho kingekuwa na wabunge wengi bungeni, na
kingeunda Serikali.
Mwanasiasa
anayeupuuza uhalisia huu hawezi kuwa mwanasiasa makini. Nchi hii
inahitaji siasa za upinzani. Inahitaji uwepo wa wabunge wengi wa
upinzani bungeni. Lakini, kazi kubwa inahitajika, na zaidi kujenga
misingi ya vyama, si mijini tu, hata vijijini. Na kukubali kuwa, wapiga
kura wa leo si wajinga. Wanahitaji uwepo wa Serikali himilivu- Stable
Government. Na uhimilivu huo uanze kuonekana kwenye vyama vyenyewe na
hususan kwenye demokrasia ya ndani ya vyama- Intra-party democracy.
Muhimu ni kuyaona sasa mapungufu na kuanza kazi ya kujisahihisha. Inawezekana.
Maggid.
Post a Comment