Unknown Unknown Author
Title: ZUMA KUJIELEZA KUHUSU NYUMBA YAKE
Author: Unknown
Rating 5 of 5 Des:
Nyumba hii iligharimu dola milioni 23 kwa ukarabati Rais Jacob Zuma anatarajiwa kufika mbele ya kamati ya Bunge la A-Kusini kuji...

Nyumba hii iligharimu dola milioni 23 kwa ukarabati
Rais Jacob Zuma anatarajiwa kufika mbele ya kamati ya Bunge la A-Kusini kujieleza kuhusu kashfa ya kufuja pesa za umma zilizotumiwa kukarabati nyumba yake ya kifahari.
Ukarabati huo uligharimu dola million 23 na Bw Zuma ameamrishwa na mkaguzi au mlinzi wa mali ya umma nchini humo alipe baadhi ya pesa hizo .
Zuma alisema Jumatatu kuwa sio sawa kwake kutakiwa alipe sehemu ya pesa zilizotumiwa kwa ukarabati wa nyumba yake kwani sio yeye aliayeamuru ukarabati huo.
Alisema kuwa maafisa wa serikali ndio walioagiza ukarabati huo bila ya kumshauri.
Zuma alizungumza kwa mara ya kwanza Jumatatu tangu kashfa hiyo kujulikana akisema kuwa halipi chochote kwani hakuomba ukarabatai kufanywa.
Chanzo:BBC
Mjumbe Jr

About Author

Advertisement

Post a Comment

 
Top