Unknown Unknown Author
Title: WAOMBAJI 10800 WAPITISHWA KUWANIA NAFASI 70 TU UHAMIAJI!
Author: Unknown
Rating 5 of 5 Des:
Pichani juu;Ofisi ya Uhamiaji Mkoa wa Rukwa Ndugu zangu, hali ya ajira nchini ni mbaya sana. Idara ya Uhamiaji imetangaza nafasi z...

Pichani juu;Ofisi ya Uhamiaji Mkoa wa Rukwa


Ndugu zangu, hali ya ajira nchini ni mbaya sana. Idara ya Uhamiaji imetangaza nafasi za kazi 70 kwa wahitimu wenye shahada moja na kuendelea. Matokeo yake, baada ya mchujo wa majina zaidi ya 20,000; uongozi wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, umepitisha majina ya waombaji 10,800 ili washindanie hizo nafasi 70.

Kwa mara ya kwanza katika hostoria ya Tanzania, usaili kwa ajili ya kujaza nafasi hizo 70 utafanywa katika Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam mnamo Juni 13, mwaka huu saa 1:30 asubuhi! Hii haijawahi kutokea.

My Take:
Tatizo la ajira kweli ni janga la kitaifa kwa sasa. Hawa vijana wote wanaohitimu bila kuwa na kazi za kufanya, ni hatari sana kwa usalama wa nchi kwa sababu sidhani kama watakubali kuendelea kusota mitaani ilhali wakiwa hawana ajira. Tujadili jambo hili ili kuona namna nzuri ya kukabiliana nalo.

Nawasilisha

NB:
List kamili HII HAPA

Endelea Kututembelea Mtandaoni kwa Kuandika Neno MJUMBE BLOG na Kuingia Hapo Ili Kupata Habari,Picha na Matukio Mbali mabali ndani na Nje ya Nchi Mara kwa Mara!

MJUMBE Sr

About Author

Advertisement

Post a Comment

 
Top